Ads (728x90)

Powered by Blogger.




Familia nyingi duniani husubiri kwa hamu kubwa usiku wa kuamkia Mwaka Mpya. Usiku huo watu hujikusanya katika maeneo tofauti huku wakiimba nyimbo mbali mbali za kufurahia kuona mwaka mwingine, hata wale ambao kwa kipindi cha mwaka mzima walikuwa mbali na Mungu husikika wakilitaja jina lake kwa heshima kubwa. 


Katika orodha ya sherehe maarufu dunia, moja wapo ni sherehe ya mwaka mpya. Gazeti pendwa la Mwenge linakuletea asili ya mwaka mpya na mkanganyiko wa kimahesabu uliopelekea miaka sita kupungua.

Maadhimisho ya kwanza ya sherehe za Mwaka Mpya yalishuhudiwa huko Mesopotamia miaka 2018 iliyopita. Ilisherehekewa na Wamisri, Waajemi na Wafoeniki katika zama za Equinox katikati ya mwezi Machi, Wayunani walisherehekea katika kipindi cha majira ya baridi. Kwa mujibu wa kalenda ya kale ya Kirumi Mwaka Mpya uliangukia Machi 1, Kalenda hiyo ilikuwa na miezi kumi tu na Machi ilikuwa mwezi wa kwanza wa mwaka. Kalenda hii asili yake ni mzunguko wa mwezi, ikianzia majira ya kuchipua na kumalizia na majira ya vuli.

Numa Pompilius, mfalme wa pili wa Roma ndiye aliyeugawa mwaka katika miezi kumi na mbili ya mzunguko wa jua na kuongeza miezi ya Januari na Februari. Mwaka Mpya ukabadilishwa na kuwa Januari kutokana na mwezi huo kusadifu mwanzo wa miaka ya kiraia huko Roma.

Kaizari wa Roma Julius Caesar alitangaza rasmi kuwa Januari mosi ndio mwaka mpya ilikuwa mwaka 46 B.C. Warumi walikuwa wakimwabudu Mungu Janus ambaye alikuwa na nyuso mbili, moja ikiangalia mbele na nyingine ikiangalia nyuma. Mwezi wa Januari ulipewa jina la Mungu huyo wa Kirumi na kumpa Kaisari wazo la kuanzisha Januari kama mlango na Mwaka Mpya.

Inasemekana kuwa Kaisari aliisherehekea Januari mosi, kama mwaka mpya kwa kuamuru majeshi ya mapinduzi ya Wayahudi kurudi nyuma. Waliadhimisha mwanzo wa mwaka kwa kurejesha sheria za zamani kabla ya amani kuenea. Watu wakajua kuwa Januari ndiyo mwezi wa kwanza wa mwaka.

Katika kipindi  cha zama za kati, sikukuu za Kipagani zilipewa umuhimu mkubwa na Machi 25 ilitangazwa kama mwanzo wa Mwaka Mpya. Machi 25 iliitwa kuwa ni  Siku ya Kupashwa habari Bikira Maria na Gabrieli kwamba atamzaa Yesu Kristo (Annunciation Day). Baadaye, Malkia wa Uingereza alitangaza kuwa tarehe 25 Disemba, yaani siku aliyozaliwa Yesu lazima iadhimishwe kama Mwaka Mpya.


Takriban miaka 500 baadaye, Papa Gregory XIII aliipiga marufuku kalenda ya zamani ya Julian na kuanzisha kalenda ya Gregori ambayo ilijumuisha mwaka mrefu wenye siku 366 ambao mwezi wa Februari unakuwa na siku 29  na 28 ili kuleta uwiano kati ya misimu na kalenda. Hatimaye, mnamo mwaka 1582, kalenda ya Gregori ilianzishwa na kusherehekea Mwaka Mpya, siku ya kwanza ya Januari.

Yesu alizaliwa katika Betrehemu mwaka 6 au 7 kabla ya Kristo (BC), tunaweza kueleza kwa urahisi kwamba wakati alipozaliwa watu walihesabu miaka yao kutoka mwanzo wa mji wa Roma. Lakini Mtawa  Dionyius Exiquus, alianza kuhesabu miaka toka alipozaliwa Yesu na ukaitwa Mwaka wa Kwanza, kadiri ya hesabu za kuzaliwa kwake toka Roma ni miaka 754.

Kadiri ya Mt.2 tunaona ya kwamba Yesu alikuwa na miaka 2-3 wakati alipokufa. Mfalme Herode naye alikufa mwaka wa nne kabla ya Kristo (BC)

Hata hivyo maelezo ya Biblia yanaonesha kwamba Mtawa Dionysius Exiquus ambaye alipewa jukumu la kufanya mahesabu   ya miaka, kuna makosa aliyafanya katika mahesabu ambapo alisahau kuhesabia kati ya miaka 6 au 7 ( The Results of false Calculations), makosa ambayo inaelezwa yalifanyika kwenye  karne ya sita, kwa kuwa inakadiliwa Yesu alizaliwa kati kati ya 7BC  na 2BC. 
Mtawa Dionysius Exiquus alizaliwa 470 C.AD huko Scythia Mashariki mwa milki ya Roman na alifariki dunia 544 AD Roma, Italy. Kutoka na mkanganyiko huu, kwa kuzingatia maelezo ya kitabu kitakatifu cha Mwenyenzi Mungu yaani Biblia, ni wazi kwamba Miaka 6 ilisahaulika, hivyo 2018 tukiongeza miaka 6 jumla yake tunapata miaka 2024.

Basi kila mmoja wetu anaweza akaongezea lakini ni ngumu kubadiri hesabu ya sasa ya 2018 kwa kuwa imeshakubarika na inatumiwa na wanadamu wote licha ya kwamba katika uislamu wanamfumo wao tofauti wa jinsi ya kuhesabu miaka yao. 

Mwaka mpya wa kiislamu ambao unafupishwa kama H au Hijriyyah, tarehe 01 Muharram H ilikuwa ni sawa na tarehe 16 Julai 622 M. Na inatamburika hivyo mpaka leo. Historia inasema miaka ya kiislamu imeanza kuhesabika baada ya Maswahaba kuhama kutoka Makkah kwenda Madiynah, lakini mfumo uliokubarika kimataifa wa kuhesabu miaka ni huu wa baada ya Yesu Kristo kuzaliwa.

Mwaka 2018 umeanza na sisi sote bado tuna kamba mguuni, nikiwa na maana ya ugeni wetu katika mwaka huu, inatupasa kutafakari kwa kina kihusu wajibu wetu wa hapa duniani jinsi tutakavyoingia mbinguni kwa lengo la kuurithi ufalme wa Mungu. 

Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha, ndio maana kila baada ya mienzi 12 tunasherekea mwaka mpya. Hata maisha yetu yanaukomo vile vile,  lazima tusali na kumwomba Mwenyezi Mungu daima, kwa kuwa hatujui muda wala saa pale mwana wa Adam atakapokuja kutuchukua, Amina!


Post a Comment